المدة الزمنية 4:18

Rais Magufuli apiga msumali wa mwisho sakata la makontena ya RC Makonda

بواسطة Azam TV
119 095 مشاهدة
0
357
تم نشره في 2018/08/30

Rais Magufuli hatimaye amekata mzizi wa fitna kuhusiana na makontena Ishirini yanayoshikiliwa Bandarini Jijini Dar Es Salaam yakidaiwa kuwa na samani za shule yaliyoletwa kwa msaada kwa jina la Mkuu wa Mkoa wa Dar Es Salaam Paul Makonda akisema ni lazima yalipiwe kodi. Dokta Magufuli amesema kwamba makontena hayo yanayodaiwa kodi yenye thamani ya Bilioni Moja Nukta Mbili yanapaswa kulipiwa kodi hiyo kwa sababu aliyeletewa hana mamlaka ya kisheria ya kupata msamaha huku pia akihoji ni kwa nini shule zinazopelekewa samani hizo hazijatajwa. Rais Dokta Magufuli amezungumza hayo akiwa Chato Mkoani Geita alipokutana kwa mazungumzo na Viongozi na Wafanyakazi wa Halmashauri ya Wilaya ya Chato.

الفئة

عرض المزيد

تعليقات - 38